Tuesday, September 13, 2016

KATIKA KUHAKIKISHA WANANCHI WA PANGANI WANAPATA MAJI SAFI MBUNGE SAUMU SAKALA ATEMBELE KITONGOJI CHA KWANG'OMBE





Katika kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama mbunge wa viti maalum Pangani SAUMU SAKALA ametembelea kijiji cha mikinguni kitongoji cha kwang’ombe kuona jinsi gani atawasaidia wanakijiji hao kupata maji safi na salama.

Wananchi hao wamesemakuwa wamechimbiwa kisima na Islamic Help lakini maji ya kisima hicho ni ya chumvi na hayafai kwa kunywa.
Hivyo inawabidi kutembea umbali mrefu hadi katika vijiji vyenye maji safi kwa ajili ya kunywa ikiwemo kijiji cha ushongo,mikinguni,na kasanga   kwaajili ya kupata maji ya kunywa .

Hatahivyo kwa wanakijiji ambao wanashindwa kutembea katika vijiji vyenye maji safi kwaajili ya kunywa hulazimika kunywa maji ya chumvi yanayo patikana kasima na wengine hufikia hatua ya kunywa maji yanayo tumiwa kunyweshea mifugo.
kwaupande wake Mwenyekiti wa kitongoji RUKIA HAMZA amekiri kuwepo kwa shida ya maji katika kitongoji chake lakini wameshindwa namna ya kufikisha maji kutoka mikinguni mjini hadi kitongoji cha kwang’ombe.

Pia Mtendaji wa kjiji cha mikinguni SALIMU MWAIPOPO amesema walishalifuatilia suala la ukosefu wa maji ya kunywa katika kitongiji cha kwang’ombe katika idara ya maji pangani na watu kutoka idara ya maji walishapima lakini umepita muda mrefu hadi sasa bado hawajapewa mrejesho juu ya gharama ya kutoa maji kutoka mikinguni hadi kufika katika kitongoji hicho.

Hivyo (1)ombila lao kwa Mh SAUMU SAKALA ni kuwasaidia gharama za kutoa maji kutoka mkinguni mjini hadi katika kitongoji cha kwang’ombe.(2)pia wamegundua hapo hapo katika kitongoji cha kwang’ombe kunasehemu kuna maji ya baridi ambayo hayana chumvi hivyo wamependekeza kama gharama zitakua kubwa za kutoa maji kutoka mikinguni basi wachimbiwe kisima katika eneo ambalo lina maji mazuri kwa matumizi ya kunywa.

Share:

Hon. Saumu Heri Sakala

Hon. Saumu Heri Sakala
Member of Parliment (MP)

Video

Recent Posts