Friday, August 12, 2016

YALIO JIRI ZIARA YA MBUNGE SAUMU SAKALA KATA ZA SIGAYA,BOMA,MKINGA MJINI, NA KATA YA KWALE WILAYANI MKINGA




 
Mbunge Saumu Sakala akikagua Jengo la Shule iliyo Jengwa kupitia nguvu za wananchi katika kata ya Sigaya Wilayani Mkinga





Mbunge Saumu Sakala amendelea na ziara ya kata kwa kata wilaya kwa wilaya katikawilaya ya mkinga kata ya sigaya.
Katika ziara hiyo aliongozana na wenyeviti na diwani wa viti maalum kujua changamoto zinazo wakabili wanakijiji wa kata ya sigaya iliyoko wilaya ya mkinga.
Mbunge amejionea changamoto ya wahamiaji haramu kutoka kenya  inayo wakabili wakazi wa kata hiyo,ambapo wahamiaji hao wamekua wakiharibu mazingira kwa kukata miti na kwenda kuuza kenya.
Wananchi hao pia wamelalamikia suala la wizi wa mifugo unao fanywa na wahamiaji hao huku wakisema wahamiaji ni kutoka kabila la waduruma na wakamba ambao baada ya kuiba mifugo huenda kuuza kenya.
Kunyang’anywa kwa vitambulisho vya ukazi kwa baadhi ya raia ambao ni WATANZANIA huku mamlaka husika wilayani mkinga ikidai ni wahamiaji kutoka kenya.
Pia wananchi wa kata ya sigaya wamelalamikia changamoto ya  kutokamilika kwa shule ya msingi iloiyojengwa kupitia nguvu za wananchi,vyoo pamoja na kutokamilika kwa nyumba za wauguzi katika kata hiyo .
Suala ambalo Mbunge Saumu Sakala amehuzunika sana  hatua ya shule iliyojengwa kupitia nguvu za wananchi na serikali kushindwa kuwasidia wananchi hao kukamilisha shule hiyo.
Lakini kufuatia changamoto hizo Mh Mbunge Saumu Sakala ameahidi kufuatilia matatizo hayo na kuwaambia wana kata ya sigaya kuwa atakutana na Waziri wa mambo ya ndani juu ya kupambana na suala la wahamiaji haramu kutoka kenya.
Pia mbunge saumu sakala aliendelea na ziara yake katika kata tatu ambazi ni kata ya Boma Ndani ,Mkinga Mjini,na kumalizia katika kata ya kwale ambapo alikutana na chamgamotom nyingi ambazo kwanamna moja ama nyingine zinarudisha maendeleo ya wilayaya mkinga.
Miongoni mwa changamoto hizo ni ubovu wa barabara katika kata ya Boma Ndani ambayo kwa wakati wa mvua watoto wa shule huwawanashindwa kwenda shule.
Suala la ambalo Diwani wa Kata hiyo Nasir Salim Saum amesema yuko katika hatua mwisho ya ufuatiliaji kwani mara nyingi amekua akiipigia kelele lakini changamoto ni ilikua pesa hakuna hivyo ameahidiwa na halmashauri kuwa wataifanyia marekebisho barabara hiyo.
Hatahivyo kwa upande wa Mbunge Saumu Sakala amewaambia wananchi katika kata hiyo wawe kitu kimoja katika kuijenga kata yao na pele wanaona ugumu wasiache kumshirikisha kwani nyeye yupo kwaajili ya kuwatumukia wao.
Share:

Hon. Saumu Heri Sakala

Hon. Saumu Heri Sakala
Member of Parliment (MP)

Video

Recent Posts