Monday, October 3, 2016

MBUNGE SAUMU SAKALA AWAWEZESHA WAKIMAMA WA PANGANI KUPATA MAFUNZO YA KUANZISHA NA KUVIENDELEZA VIKOBA NA MIFUKO YA KIJAMII



Katika kuhakikisha kinamama wa pangani wanapata mafunzo ya kuanzisha na  kuviendeleza  vikoba  na mifuko ya jamii , leo Mbunge wa Viti Maalumu Pangani SAUMU SAKALA ametimiza ahadi yake ya kumleta mwalimu kwa lengo la kutoa elimu kwa wakinamama.

Mafunzo hayo yameanza kutolewa leo katika shule ya msingi funguni ambayo yalihudhuriwa na vikundi vitatu vya wakina mama kikiwemo kikundi cha Amani Group,Jitihada na kikundi cha Muungano.

Ambapo katika mafunzo hayo kinamama wenyewe wamekiri kutokuwa na uelewa wa kuviendeleza vikundi vyao na kusemakuwa kutokana na mafunzo ambayo wameanza kuyapata leo yamewapa mwanganza katika kuviendeleza vikundi vyao .

Halikadhalika mafunzo hayo yalihudhuriwa na diwani wa pangani mashariki Mh AKIDA BORAMIMI ambapo amewataka wakina mama  kuzingatia mafunzo wanayopata kutoka kwa muwezeshaji wa mafunzi hayo mwalimu JULIASI NGOMA .

Pia Mh AKIDA BORAMIMI amewaomba kinamama kuwahi mapema katika mafunzo hayo ilikuweza kupata ufahamu juu ya uanzishaji na uendeshaji wa vikoba kwa lengo la kuwapatija wakinamama Wa PANGANI.
Mafunzo ya kuwapa kinamama elimu juu ya kuanzisha na kuviendeleza vikoba ama mifuko ya kijamii kwa
wakinamama wa Pangani yameanza leo na yatatarajiwa kuisha tarehe 5/10/2016.

Share:

Hon. Saumu Heri Sakala

Hon. Saumu Heri Sakala
Member of Parliment (MP)

Video

Recent Posts