Friday, August 12, 2016

MBUNGE SAUMU SAKALA AENDELEA NA ZIARA KATA YA DALUNI NA MARAMBA WILYANI MKINGA


Msingi wa ujenzi wa Zahanati ya Kata ya Daluni uliogharimu shilingi Milioni 8 ambao kwa sasa umekwama zaidi ya miaka miwili

Siku ya pili ya ziara ya Mbunge Saumu Sakala katika wilaya mkinga ndani ya kata ya Daluni na Kata ya Maramba ambapo lengo ni kusikliza changamoto mbalimbali zinazo wakumba wananchi wa Wilaya ya Mkinga.
Akianzia katika kata ya Daluni wakazi wa kata hiyo walifurahishwa na ziara ya Mbunge hiyo lakini hawakuacha kumpa changamoto zinazowakabili katika kata yao.
Ambapo changamoto ya Zahanati ndio ilikuwa kubwa ambayo inawafanya wakazi wa kata hiyo kutembea hadi maramba mjini ilikupata huduma hiyo.
Ambapo katika changamoto hiyo Mbunge alitakakujua mwenyekiti amelifuatiliaje suala hilo,hivyo mwenyekiti alitoa tarifa ya kukwama kwa zahanati hiyo.
Mwenyekiti wa kitongoji kata ya Daluni alisema kuwa zahanati hiyo ilipangwa kujengwa lakini mpaka sasa ujenzi huo umeishia kwenye hatua ya msingi na kwa sasa ni miaka miwili imepita kila wakilifuatila suala hilo majibu hakuna.
Pia mwenyekiti huyo alimuambie mbunge kuwa ujenzi huo mpaka sasa umetumia shilingi milioni 8 suala ambalo pia linawaacha wananchi mdomo wazi.
Hatahivyo Mbunge alimtaka mwenyekiti kuatilia tena suala hilo kwani haiwezekani kiasi kikubwa cha pesa kimetumika na zahanati ipo katika hatua ya msingi.
Vilevile katika hatua nyingine wananchi hao wamelalamikia suala la kuto patikana na huduma ya kupatikana kwa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto na kusema kuwa wanalazimika kutembea hadi mkinga mjini.
Hivyo walimtaka Mbunge kuwaombea huduma hiyo kusogozewa karibu kwani usumbufu wanaokutana nao ni mkubwa ili kuweza kupata huduma hiyo.
Na kwa upande wake Mbunge Saumu Sakala amewaahidi wakazi wa kata ya Daluni kuwa ataongea na RITA ili kuweza kuwasogezea huduma hiyo karibu wakazi wa daluni hata kwa mwezi mara ,moja ilikuweza kuwaondolea wakazi hao usumbufu huo.
Pia changamoto ya kukosekana kwa Tenki ya kuhifadhiwa maziwa hatua inayosababisha wafugaji wa kata ya Daluni kutembea hadi maramba kupeleka maziwa yao.
Hivyo walimtaka Mbunge awafuatilie suala la hilo katika uongozi wa Tanga Fresh ili waweze kupata Tenki hiyo.
Halikadhalika katika kata ya Maramba vitu vilivyo jitokeza ni kuuzwa kwa mbao ambazo zilikatwa kwa lengo la kutengenezwa kwa mdawati ya shule ya Maramba.
Na changamoto inayo wakwamisha ni kukosa fedha ya nauli ambayo itawafikisha hadi kwa mkurugenzi na mkuu wa wilaya ilikulifuatilia suala la kuuzwa kwa mbao hizo.
Hivyo Mbunge aliwawezesha Fedha ya nauli nakuwaambia kwa kilahatua watakayo fika wamjulishe na pia mbunge amewaahidikuwapa ushirikiano juu ya kutatua suala hilo.
Ziara ya Mbunge Saumu Sakala iliishia katika kata ya Maramba na kata ya Daluni ambapo ameahidi kuyafuatilia yale yote ambao wamempa kwa lengo ya kuyatatua,

Share:

Hon. Saumu Heri Sakala

Hon. Saumu Heri Sakala
Member of Parliment (MP)

Video

Recent Posts