Monday, August 8, 2016

UVUVI HARAMAU BADO KIZUNGUMKUTI PANGANI TANGA



Wadau wa uvuvi wilayani pangani wamesikitishwa na namna idara ya uvuvi wilaya humo inavyolishuhuliki suala la uvuvi haramu.
Akiongea na Saumusakalamp.blogspot.com mmoja wa wavuvi wilaya ya pangani Ndugu 
KIMWERI ALI amesema kuwa uvuvi wa kutumia baruti imekua ukitumika katika miamba ya bahari ya pangani lakini idara ya uvuvi mpaka sasa haijachukua hatua yoyote kukabiliana na suala hilo.
KIMWERI Ameogeza kuwa wamekua wakitoa taarifa kwa idara hiyo juu ya matukia ya wavuvi wanatumia baruti katika uvuvi lakini changamoto wanayokutana nayo ni baadhi ya watu idara ya uvuvi wanamtandao na wavuvi haramu hivyo taarifa zao ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.
Kwaupande wa mwenyekiti   wa  pangani mashariki HAJI NUNDU ambaye idadi kubwa ya wakazi wake  ni wavuvi amesema kuwa mara kwa mara serikali yake imekua ikitoa taarifa kwenye idara hiyo juu ya wavuvi kutumia baruti pindi wanapokua baharini lakini majibu ya idara hiyo ni kuwa BOTI haina mafuta ama BOTI  haiko kwenye maji.
Hivyo kwa majibu mepesi ya idara hiyo inaonyesha wazi kuwa nivigumu kupambana na uvuvi haramu wilayani pangani kwakua idara husika imelala.
Kwaupande wake AMINA SULEIMAN ambaye  alikaimu mkuu wa kitengo idara ya uvuvi wilaya ya pangani amesema kuwa idara ya uvuvi inapambana na uvuvi haramu lakini changamoto ni idara hiyo inapopata taarifa juu ya wavuvi kutumia baruti baharini mara nyingi boti inakua haina mafuta na mlolongo wa kupata mafuta ni mrefu.
Hivyo ni vigumu kuwakamata wavuvi wa baruti kwasababu  mpaka unakamilisha mlolongo wa kunapata mafuta wavuvi hao wameshaondoka.
Pia boti ya inayotumiwa na idara hiyo mara nyingi inakua haina mafuta ya hakiba kwaajili ya matumizi ya dharura .
Share:

Hon. Saumu Heri Sakala

Hon. Saumu Heri Sakala
Member of Parliment (MP)

Video

Recent Posts