.

..

.

..

.

..

.

..

.

..

Thursday, October 6, 2016

ALICHOKISEMA MWALIMU WA MAFUNZO YA VIKOBA PANGANI

Share:

Wednesday, October 5, 2016

MANENO YA DIWANI AKIDA BORAMIMI AKIFUNGA MAFUNZO YA VIKOBA PANGANI

Share:

Monday, October 3, 2016

MBUNGE SAUMU SAKALA AWAWEZESHA WAKIMAMA WA PANGANI KUPATA MAFUNZO YA KUANZISHA NA KUVIENDELEZA VIKOBA NA MIFUKO YA KIJAMII



Katika kuhakikisha kinamama wa pangani wanapata mafunzo ya kuanzisha na  kuviendeleza  vikoba  na mifuko ya jamii , leo Mbunge wa Viti Maalumu Pangani SAUMU SAKALA ametimiza ahadi yake ya kumleta mwalimu kwa lengo la kutoa elimu kwa wakinamama.

Mafunzo hayo yameanza kutolewa leo katika shule ya msingi funguni ambayo yalihudhuriwa na vikundi vitatu vya wakina mama kikiwemo kikundi cha Amani Group,Jitihada na kikundi cha Muungano.

Ambapo katika mafunzo hayo kinamama wenyewe wamekiri kutokuwa na uelewa wa kuviendeleza vikundi vyao na kusemakuwa kutokana na mafunzo ambayo wameanza kuyapata leo yamewapa mwanganza katika kuviendeleza vikundi vyao .

Halikadhalika mafunzo hayo yalihudhuriwa na diwani wa pangani mashariki Mh AKIDA BORAMIMI ambapo amewataka wakina mama  kuzingatia mafunzo wanayopata kutoka kwa muwezeshaji wa mafunzi hayo mwalimu JULIASI NGOMA .

Pia Mh AKIDA BORAMIMI amewaomba kinamama kuwahi mapema katika mafunzo hayo ilikuweza kupata ufahamu juu ya uanzishaji na uendeshaji wa vikoba kwa lengo la kuwapatija wakinamama Wa PANGANI.
Mafunzo ya kuwapa kinamama elimu juu ya kuanzisha na kuviendeleza vikoba ama mifuko ya kijamii kwa
wakinamama wa Pangani yameanza leo na yatatarajiwa kuisha tarehe 5/10/2016.

Share:

Friday, September 23, 2016

MBUNGE SAUMU SAKALA ,JUMAA HAMIDU AWESO NA MKUU WA WILAYA PANGA BI ZAINABU WASUKUMA MBELE HARAMBEE YA KINAMAMA PANGANI


Mkuu wa wilaya ya pangani Bi Zainabu Abdallah akiwa pamoja na Mbunge wa viti maalum Saumu Sakala,na Mbunge wa jimbo la Pangani Jumaa Hamidu Aweso katika Harambee ya kuwachingia wakina mama wa kikundi cha AMANI GROUP cha Pangani Magharibi.

 Katika kuhakikisha kina mama wilaya ya pangani wanasonga mbele kimaendeleo leo kinamama wa kikundi cha AMANI GROUP cha Pangani Magharibi wameitisha kikao huku lengo la kikao hicho ni kufanya harambee ili kuwasaidia kinamama hao.


Na katika harambee hiyo iliyo hudhuruwa na Wabunge wa wilaya ya Pangani Mh Saumu Sakala na Mh Jumaa Hamidu Aweso huku Mkuu wa Wilaya ya Pangani Bi Zainabu Abdallah akiwa ndio mgeni mualikwa wa harambee hiyo.
Na huku Bi zainabu akiendesha harambee hiyo, Mbunge wa viti maalum Pangani Saumu Sakala ametoa  shilingi laki mbili,Mbunge Jumaa Hamidu Aweso ametoa laki tatu,mwenyekiti wa kata ya pangani magharibi laki tatu,katibu wa wafugaji wilaya laki mbili huku viongozi wengine wa vyama wakitoa fedha katika harambee hiyo.
Pia katika harambee hiyo Mbunge saumu sakala ameahidi kuwaletea wakinamama wa kikundi cha Amani Group Mwalimu wa kuwafundisha Ujasiria mali ili kipato cha wakinamama hao kuongezeka .

Na kwaupande wake Mbunge Jumaa Hamidu Aweso wakati akitoa neno katika harambee hiyo amewataka wakina mama hao kuandika barua ili kuweza kupa fedha zinazo tokana na mfuko wa jimbo.
kwaupande wake mkuu wa wilaya ya Pangani Bi Zainabu amewapongeza wakinamama hao kwaku thubutu kuanzisha kikundi chao kwa lengo la kuwakwamua wakina mama.
Lakini amewataka wakinamama hao kukisajili kikundi chao halmashauri ili hata wakati wa kutoka asilimia 5 ya halmashauri na wao wawezekupata fedha kwaajili ya maendeleo ya kikundi hicho.
Hatahivyo Bi Zainabu hakuwacha kuwashukuru wabunge kwakuacha mda wao na kukubali kuja katika harambee ya kikundi cha kinamama cha Amani Group cha Pangani Magaribi,na huku  akiwaomba kuwa pamoja katika kupeleka maendeleo ya Pangani mbele.
Hivyo  katika harambee hiyo ya kikundi cha kina mama cha Amani Group mkuu wa wilaya Bi Zainabu ametaja fedha zilizo patikana ni shililngi Milioni Moja Laki Saba na Elfu Arubaini Kwaajili ya kuwasaidia wakina mama hao.

Share:

Tuesday, September 13, 2016

KATIKA KUHAKIKISHA WANANCHI WA PANGANI WANAPATA MAJI SAFI MBUNGE SAUMU SAKALA ATEMBELE KITONGOJI CHA KWANG'OMBE





Katika kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na salama mbunge wa viti maalum Pangani SAUMU SAKALA ametembelea kijiji cha mikinguni kitongoji cha kwang’ombe kuona jinsi gani atawasaidia wanakijiji hao kupata maji safi na salama.

Wananchi hao wamesemakuwa wamechimbiwa kisima na Islamic Help lakini maji ya kisima hicho ni ya chumvi na hayafai kwa kunywa.
Hivyo inawabidi kutembea umbali mrefu hadi katika vijiji vyenye maji safi kwa ajili ya kunywa ikiwemo kijiji cha ushongo,mikinguni,na kasanga   kwaajili ya kupata maji ya kunywa .

Hatahivyo kwa wanakijiji ambao wanashindwa kutembea katika vijiji vyenye maji safi kwaajili ya kunywa hulazimika kunywa maji ya chumvi yanayo patikana kasima na wengine hufikia hatua ya kunywa maji yanayo tumiwa kunyweshea mifugo.
kwaupande wake Mwenyekiti wa kitongoji RUKIA HAMZA amekiri kuwepo kwa shida ya maji katika kitongoji chake lakini wameshindwa namna ya kufikisha maji kutoka mikinguni mjini hadi kitongoji cha kwang’ombe.

Pia Mtendaji wa kjiji cha mikinguni SALIMU MWAIPOPO amesema walishalifuatilia suala la ukosefu wa maji ya kunywa katika kitongiji cha kwang’ombe katika idara ya maji pangani na watu kutoka idara ya maji walishapima lakini umepita muda mrefu hadi sasa bado hawajapewa mrejesho juu ya gharama ya kutoa maji kutoka mikinguni hadi kufika katika kitongoji hicho.

Hivyo (1)ombila lao kwa Mh SAUMU SAKALA ni kuwasaidia gharama za kutoa maji kutoka mkinguni mjini hadi katika kitongoji cha kwang’ombe.(2)pia wamegundua hapo hapo katika kitongoji cha kwang’ombe kunasehemu kuna maji ya baridi ambayo hayana chumvi hivyo wamependekeza kama gharama zitakua kubwa za kutoa maji kutoka mikinguni basi wachimbiwe kisima katika eneo ambalo lina maji mazuri kwa matumizi ya kunywa.

Share:

Wednesday, August 17, 2016

IJUE SABABU YA MBUNGE WA JIMBO LA TANGA MUSSA MBAROK KUKAMATWA NA POLISI

Share:

IJUE SABABU YA MBUNGE WA JIMBO LA TANGA MUSSA MBAROK KUKAMATWA NA POLISI

Share:

Friday, August 12, 2016

MBUNGE SAUMU SAKALA AMEANZA KUFUATILIA CHANGAMOTO ZA WANANCHI WA DALUNI -TANGA FRESH




 
Mbunge SAUMU SAKALA amenza kufuatilia changamoto alilzokutana nazo katika ziara yake wilayani mkinga katika Kata ya Daluni.
Leo mbunge Sakala amekwenda katika kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh kufuatilia suala la kupelekwa kwa mtungi wa maziwa kero ambayo imekua ikiwalazimu wakazi wa Daluni kupeleka maziwa Maramba mjini.
Akiongea na mkuu wa kitengo cha kusambaza Tenki hizo kwenye vituo ADAM NYEREMBE GAMBA amesema kuwa amefurahishwa na hatua ya mbunge huyo kufuatilia suala hilo lakini kwa sasa Tanga Fresh imekubwa na tatizo la kifedha hivyo kunaugumu wa kutekeleza ombi hilo.
Adam amesema kuweka mtungi ni gharama kubwa sana na pia mitungi hiyo haipatikani hapa nchini, kwani mitungi hiyo inaagizwa kutoka nje ya nchi,hivyo nivigumu kuagiza mtungi mmoja.
Hivyo mkuu huyo wakitengo amewataka wafugaji wa Daluni kupeleka maziwa yao Maramba kama hapo awali walivyo kuwa wakifanya.
Pia kiwanda kipo katika urekebishaji wa mfumo wa maji taka ambao urekebishwaji wake unagharimu pesa nyingi sana ni Zaidi ya milioni 350.
Na wasipo rekebisha mfumo huo kuna hatari ya kiwanda hicjo kufungiwa uzalishaji kwani walishapewa notes na waziri wa mazingira kurekebisha mvumo wao wa maji taka
Pia kutokana upatikanaji wa maziwa mengi katika wakati wa vuli hivyo kiwanda kimepanga kufanya upanuzi wa kiwanda hicho na ujenzi huo utagharimu shilingi bilioni 12,hivyo utaona pesa itakayo tumika ni nyingi.
Hivyo Adam amewataka wakazi wa Kata ya Daluni kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho kiwanda cha Tanga fresh kipo katika hali mbaya ya kifedha na pindi mambo yakiwa mazuri watapa Mtungu huo wa Maziwa.

Share:

Hon. Saumu Heri Sakala

Hon. Saumu Heri Sakala
Member of Parliment (MP)

Video

Recent Posts