Thursday, October 6, 2016
Wednesday, October 5, 2016
Monday, October 3, 2016
MBUNGE SAUMU SAKALA AWAWEZESHA WAKIMAMA WA PANGANI KUPATA MAFUNZO YA KUANZISHA NA KUVIENDELEZA VIKOBA NA MIFUKO YA KIJAMII
Mafunzo hayo yameanza kutolewa
leo katika shule ya msingi funguni ambayo yalihudhuriwa na vikundi vitatu vya
wakina mama kikiwemo kikundi cha Amani Group,Jitihada na kikundi cha Muungano.
Ambapo katika mafunzo hayo
kinamama wenyewe wamekiri kutokuwa na uelewa wa kuviendeleza vikundi vyao na
kusemakuwa kutokana na mafunzo ambayo wameanza kuyapata leo yamewapa mwanganza
katika kuviendeleza vikundi vyao .
Halikadhalika mafunzo hayo
yalihudhuriwa na diwani wa pangani mashariki Mh AKIDA BORAMIMI ambapo amewataka
wakina mama kuzingatia mafunzo
wanayopata kutoka kwa muwezeshaji wa mafunzi hayo mwalimu JULIASI NGOMA .
Mafunzo ya kuwapa kinamama elimu
juu ya kuanzisha na kuviendeleza vikoba ama mifuko ya kijamii kwa
wakinamama wa
Pangani yameanza leo na yatatarajiwa kuisha tarehe 5/10/2016.Friday, September 23, 2016
MBUNGE SAUMU SAKALA ,JUMAA HAMIDU AWESO NA MKUU WA WILAYA PANGA BI ZAINABU WASUKUMA MBELE HARAMBEE YA KINAMAMA PANGANI
Katika kuhakikisha kina mama wilaya ya pangani wanasonga mbele kimaendeleo leo kinamama wa kikundi cha AMANI GROUP cha Pangani Magharibi wameitisha kikao huku lengo la kikao hicho ni kufanya harambee ili kuwasaidia kinamama hao.
Na huku Bi zainabu akiendesha harambee
hiyo, Mbunge wa viti maalum Pangani Saumu Sakala ametoa shilingi laki mbili,Mbunge Jumaa Hamidu Aweso
ametoa laki tatu,mwenyekiti wa kata ya pangani magharibi laki tatu,katibu wa
wafugaji wilaya laki mbili huku viongozi wengine wa vyama wakitoa fedha katika
harambee hiyo.
Pia katika harambee hiyo Mbunge
saumu sakala ameahidi kuwaletea wakinamama wa kikundi cha Amani Group Mwalimu
wa kuwafundisha Ujasiria mali ili kipato cha wakinamama hao kuongezeka .
Na kwaupande wake Mbunge Jumaa
Hamidu Aweso wakati akitoa neno katika harambee hiyo amewataka wakina mama hao
kuandika barua ili kuweza kupa fedha zinazo tokana na mfuko wa jimbo.
kwaupande wake mkuu wa wilaya ya
Pangani Bi Zainabu amewapongeza wakinamama hao kwaku thubutu kuanzisha kikundi
chao kwa lengo la kuwakwamua wakina mama.
Lakini amewataka wakinamama hao
kukisajili kikundi chao halmashauri ili hata wakati wa kutoka asilimia 5 ya
halmashauri na wao wawezekupata fedha kwaajili ya maendeleo ya kikundi hicho.
Hatahivyo Bi Zainabu hakuwacha
kuwashukuru wabunge kwakuacha mda wao na kukubali kuja katika harambee ya
kikundi cha kinamama cha Amani Group cha Pangani Magaribi,na huku akiwaomba kuwa pamoja katika kupeleka
maendeleo ya Pangani mbele.
Hivyo katika harambee hiyo ya kikundi cha kina mama
cha Amani Group mkuu wa wilaya Bi Zainabu ametaja fedha zilizo patikana ni
shililngi Milioni Moja Laki Saba na Elfu Arubaini Kwaajili ya kuwasaidia wakina
mama hao.
Tuesday, September 13, 2016
KATIKA KUHAKIKISHA WANANCHI WA PANGANI WANAPATA MAJI SAFI MBUNGE SAUMU SAKALA ATEMBELE KITONGOJI CHA KWANG'OMBE
Katika kuhakikisha
wananchi wanapata maji safi na salama mbunge wa viti maalum Pangani SAUMU
SAKALA ametembelea kijiji cha mikinguni kitongoji cha kwang’ombe kuona jinsi
gani atawasaidia wanakijiji hao kupata maji safi na salama.
Wananchi hao
wamesemakuwa wamechimbiwa kisima na Islamic Help lakini maji ya kisima hicho ni
ya chumvi na hayafai kwa kunywa.
Hivyo inawabidi
kutembea umbali mrefu hadi katika vijiji vyenye maji safi kwa ajili ya kunywa
ikiwemo kijiji cha ushongo,mikinguni,na kasanga kwaajili ya kupata maji ya kunywa .
kwaupande wake Mwenyekiti
wa kitongoji RUKIA HAMZA amekiri kuwepo kwa shida ya maji katika kitongoji
chake lakini wameshindwa namna ya kufikisha maji kutoka mikinguni mjini hadi
kitongoji cha kwang’ombe.
Pia Mtendaji wa kjiji
cha mikinguni SALIMU MWAIPOPO amesema walishalifuatilia suala la ukosefu wa
maji ya kunywa katika kitongiji cha kwang’ombe katika idara ya maji pangani na
watu kutoka idara ya maji walishapima lakini umepita muda mrefu hadi sasa bado
hawajapewa mrejesho juu ya gharama ya kutoa maji kutoka mikinguni hadi kufika
katika kitongoji hicho.
Wednesday, August 17, 2016
Friday, August 12, 2016
MBUNGE SAUMU SAKALA AMEANZA KUFUATILIA CHANGAMOTO ZA WANANCHI WA DALUNI -TANGA FRESH
Mbunge SAUMU SAKALA
amenza kufuatilia changamoto alilzokutana nazo katika ziara yake wilayani
mkinga katika Kata ya Daluni.
Leo mbunge Sakala
amekwenda katika kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh kufuatilia suala la
kupelekwa kwa mtungi wa maziwa kero ambayo imekua ikiwalazimu wakazi wa Daluni
kupeleka maziwa Maramba mjini.
Akiongea na mkuu wa
kitengo cha kusambaza Tenki hizo kwenye vituo ADAM NYEREMBE GAMBA amesema kuwa
amefurahishwa na hatua ya mbunge huyo kufuatilia suala hilo lakini kwa sasa
Tanga Fresh imekubwa na tatizo la kifedha hivyo kunaugumu wa kutekeleza ombi
hilo.
Adam amesema kuweka
mtungi ni gharama kubwa sana na pia mitungi hiyo haipatikani hapa nchini, kwani
mitungi hiyo inaagizwa kutoka nje ya nchi,hivyo nivigumu kuagiza mtungi mmoja.
Hivyo mkuu huyo
wakitengo amewataka wafugaji wa Daluni kupeleka maziwa yao Maramba kama hapo
awali walivyo kuwa wakifanya.
Pia kiwanda kipo katika
urekebishaji wa mfumo wa maji taka ambao urekebishwaji wake unagharimu pesa
nyingi sana ni Zaidi ya milioni 350.
Na wasipo rekebisha
mfumo huo kuna hatari ya kiwanda hicjo kufungiwa uzalishaji kwani walishapewa
notes na waziri wa mazingira kurekebisha mvumo wao wa maji taka
Pia kutokana
upatikanaji wa maziwa mengi katika wakati wa vuli hivyo kiwanda kimepanga
kufanya upanuzi wa kiwanda hicho na ujenzi huo utagharimu shilingi bilioni
12,hivyo utaona pesa itakayo tumika ni nyingi.
Hivyo Adam amewataka
wakazi wa Kata ya Daluni kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho kiwanda
cha Tanga fresh kipo katika hali mbaya ya kifedha na pindi mambo yakiwa mazuri
watapa Mtungu huo wa Maziwa.