Friday, August 12, 2016

MBUNGE SAUMU SAKALA AMEANZA KUFUATILIA CHANGAMOTO ZA WANANCHI WA DALUNI -TANGA FRESH




 
Mbunge SAUMU SAKALA amenza kufuatilia changamoto alilzokutana nazo katika ziara yake wilayani mkinga katika Kata ya Daluni.
Leo mbunge Sakala amekwenda katika kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh kufuatilia suala la kupelekwa kwa mtungi wa maziwa kero ambayo imekua ikiwalazimu wakazi wa Daluni kupeleka maziwa Maramba mjini.
Akiongea na mkuu wa kitengo cha kusambaza Tenki hizo kwenye vituo ADAM NYEREMBE GAMBA amesema kuwa amefurahishwa na hatua ya mbunge huyo kufuatilia suala hilo lakini kwa sasa Tanga Fresh imekubwa na tatizo la kifedha hivyo kunaugumu wa kutekeleza ombi hilo.
Adam amesema kuweka mtungi ni gharama kubwa sana na pia mitungi hiyo haipatikani hapa nchini, kwani mitungi hiyo inaagizwa kutoka nje ya nchi,hivyo nivigumu kuagiza mtungi mmoja.
Hivyo mkuu huyo wakitengo amewataka wafugaji wa Daluni kupeleka maziwa yao Maramba kama hapo awali walivyo kuwa wakifanya.
Pia kiwanda kipo katika urekebishaji wa mfumo wa maji taka ambao urekebishwaji wake unagharimu pesa nyingi sana ni Zaidi ya milioni 350.
Na wasipo rekebisha mfumo huo kuna hatari ya kiwanda hicjo kufungiwa uzalishaji kwani walishapewa notes na waziri wa mazingira kurekebisha mvumo wao wa maji taka
Pia kutokana upatikanaji wa maziwa mengi katika wakati wa vuli hivyo kiwanda kimepanga kufanya upanuzi wa kiwanda hicho na ujenzi huo utagharimu shilingi bilioni 12,hivyo utaona pesa itakayo tumika ni nyingi.
Hivyo Adam amewataka wakazi wa Kata ya Daluni kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho kiwanda cha Tanga fresh kipo katika hali mbaya ya kifedha na pindi mambo yakiwa mazuri watapa Mtungu huo wa Maziwa.

Share:

Hon. Saumu Heri Sakala

Hon. Saumu Heri Sakala
Member of Parliment (MP)

Video

Recent Posts