Thursday, June 23, 2016

MWONGOZO WA SPIKA ULIOOMBWA NA MHESHIMIWA ALLY MOHAMED KEISSY (MB) KUHUSU MALIPO YA POSHO KWA WABUNGE

MWONGOZO WA SPIKA ULIOOMBWA NA MHESHIMIWA ALLY
MOHAMED KEISSY (MB) KUHUSU MALIPO YA POSHO
KWA WABUNGE WANAOSUSIA MJADALA WA BUNGE
LA BAJETI KWA KUTOKA UKUMBINI
WaheshimiwaWabunge, mnamotarehe 06 Juni, 2016 katikaKikao cha Thelathini na Saba (37) cha Mkutano wa Tatu wa Bunge, Mheshimiwa Ally Mohamed Keissy (Mb) aliomba Mwongozo wa Spika kuhusu Wabunge ambao wamekuwa wakisaini kwa utaratibu mpya wa Kielektroniki (Biometric Attendance Register)lakini baada ya hapo wanatoka Ukumbini bilakushiriki Mjadala wa Bunge la Bajeti unaoendelea.
Hoja ya Mhe. Keissy (Mb) ilikuwa ni kutaka kujua ni utaratibu gani utatumika kudhibiti vitendo hivi ili kuokoa fedha za Serikali inayolipwa kama posho kwa Wabunge hao wanaosusia vikao vya Bunge la Bajeti. Mhe.Keissy (Mb) alieleza kuwa kwa wiki Serikali inapoteza kiasi cha Shilingi Milioni Arobaini na Mbili Mia Saba Sitini elfu (42,760,000/=) kwa kuwalipa posho Wabunge hao wasiohudhuria vikao vya Bunge. Baada ya kuomba Mwongozo huo nilieleza kuwa nitalifuatilia suala hili kuona namna nzuri ya kulishughulikia.
Vitendo vya Waheshimiwa Wabunge kujisajili na kasha kutoka ukumbuni vimekuwa vikiendelea kwa muda mrefu mpaka sasa na jambo hilo limekuwa likipingwa na kukemewa vikali nabaadhi ya Wabunge wanaobaki ukumbini. Wabunge hao, kwa nyakati tofauti wamekuwa wakiomba Mwongozo wa Kiti kuhusu kukubalika au kutokubalika kwa vitendo hivyo.
Tarehe 27 Aprili, 2016 Mhe. Hussein Mohamed Bashe (Mb) ambaye alihoji endapo ni haki na sahihi kwa Wabunge hao kupokea posho wakati hawashiriki kutimiza wajibu wao wa Kikatiba na Kisheria. Nikijibu Mwongozo huo nililieleza Bunge kuwa, Bunge lina jukumu zito la kujadili Bajetiya nchi hivyo,kila Mbunge anaowajibu wakushiriki kikamilifu na kuchangia Bajeti jambo ambalo naamini ndicho wananchi wanachokitazamia. Aidha nilieleza kuwa, inatakiwa uandaliwe utaratibu mahsusi utakaowawezesha Waheshimiwa Wabunge kulipwa posho baada ya kutekeleza majukumu yao ipasavyo na sio kujisajili pekee.
Mnamo tarehe 30 Mei, 2016 Mhe.Dkt. Harisson George Mwakyembe (Mb) Waziri wa Katiba na Sheria nae aliomba Mwongozo kuhusu suala hilo hilo baada ya kutoridhishwa na vitendo vya Wabunge kujisajili na kasha kutoka nje ya ukumbi na kulipwa posho bila kufanya kazi. Mhe.Mwakyembe alinukuu Ibaraya 26(1) na (2) za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 ambayo inatoa nafasi kwa mtu yeyote kuhoji kuhusu vitendo vinavyofanywa kinyume na Katiba. Aidha alisisitiza kwamba, kila mtu anapaswa kupata ujira kulingana na kazi anazozifanya. Ibara ya 23(1) ya Katiba inaeleza ifuatavyo:-
“23(1)Kila mtu, bila kuwapo ubaguzi wa aina yoyote, anayo haki ya kupata ujirau naolingana na kazi yake na watu wote wanaofanya kazi kulingana na uwezo wao watapata malipo kulingana na kiasi na sifa za kazi wanazozifanya.”
Katika kujibu Mwongozo wa Mhe. Mwakyembe (Mb)niliendelea kusisitiza kwamba Mbunge anatakiwa kulipwa mshahara au posho kutokana nakuhudhuria na kushiriki mijadala Bungeni na kwa kuwa Wabunge ni wawakilishiwa wananchi katika kusimamia Serikali, kutohudhuria Bungeni na kususia kutoa mchango wamawazo ni kushindwa kutimiza wajibu wake wakibunge na kwamba si sahihi na halali kwa Mbunge kupokea posho na mshahara bila kufanya kazi.
Vilevile,Mheshimiwa Ally Mohamed Keissy(Mb) kutokana na kutoridhishwa na tabia hiyo ya Wabunge, aliwahi kuomba Mwongozo katika jambo hilo katika Kikao cha 34 siku ya tarehe 01 Juni, 2016, . Alipoona jambo hilo linaendelea na Wabunge wanaotoka ukumbini hawazingatii maelekezo ya Kiti, mnamo tarehe 06 Juni, 2016 aliomba tena Mwongozo ambao ndio huu ninaoutolea maelezo.
Waheshimiwa Wabunge,nimetafakari kwa kina kuhusu vitendo vya baadhiya Wabunge kutia saini, kuingia ukumbin na kasha kutoka nje ya ukumbi nakuona kwamba endapo tabia hii itaachwa iendelee ninaamini itafika siku ambayo Wabunge wote kwa ujumla wetu tutajisajili, kuingiau kumbini na kasha kutoka nje jambo ambalo litasababisha shughuli za Bunge kutotekelezeka na hivyo kusababisha kukiukwa kwa masharti ya Katiba yanayolipa Bunge hili majukumu ya kutekeleza.
Waheshimiwa Wabunge, Kanuni ya 5(1) ya Kanuni za Kudumuza Bunge, Toleo la Januari, 2016 inaeleza kwamba Kiti kinapaswa kuzingatia pamoja na mambo mengine, maamuzi yaawaliyaliyowahi kutole wa na Maspika wa Bunge. Katika suala hili liloombewa Mwongozo, sawa na katika miongozo yaMhe. Bashe na Mhe. Mwakyembe Bunge letu liliwahi kutoa Mwongozo kwenye suala la Wabunge kuingia ukumbini na kasha kutoka njena hivyo kutoshiriki kwenye shughu lizilizopangwa.
Nimepitia maamuzi mbalimbali yaliyowahi kutolewa na Bunge letu(Speaker’s Rulings)kuhusiana na suala kama hili, hususani kuhusu vitendo vya Wabunge kutoka Ukumbini bila kutekeleza shughuli rasmi za Bunge. Mnamo tarehe 8 Aprili, 2008, Wabunge wa Chama cha CUF walitoka Bungeni na kususia shughuli rasmi zilizokuwa zimepangwa kutekelezwa kwa siku hiyo Bungeni. Kutokana na kitendo hicho cha Wabunge wa CUF, Kiti kilitoa uamuzi ufuatao:-
“Kwa sasa natamka tu kwamba Wabunge waliotoka nje ya Ukumbi kwa shughuli zisizokuwa rasmi kwa maana ya Bunge hili basihawastahili kulipwa posho zinazohusika kwa sikuzote ambazo watakuwa nje mpaka hapo tutakapotangaza utaratibu mwingine kwa sababu waliyokwenda kuyafanya wala hayahusiani na shughuliza Bunge letu.”
Napenda kuwakumbusha Waheshimiwa Wabunge kwamba, kwa mujibu wa Kanuni ya 146(1) ya Kanuni za Bunge, Wajibu wa kwanza wa kila Mbunge ni kuhudhuria vikao vya Bunge na Kamati zake. Jambo hili linapaswa kuzingatiwa na kila mmoja wetu.
Kitendo cha baadhi ya Wabunge kutoka nje mara baada ya kujisajili na hivyo kutohudhuria vikao ni ukiukwaji wa Kanuni ya 146(1) inayomtaka kila Mbunge kutekeleza majukumu yake kwa kuhudhuria vikao vya Bunge na vikao vya Kamati.
Hivyo basi, kwa kuwa jambo hili halikubaliki na kwa kuwa miongozo kadhaa imetolewa kuwasihi Waheshimiwa Wabunge wasitoke nje ya ukumbi wa Bunge kwa shughuli zisizo rasmi, lakini vitendo hivyo vimekuwa vikiendelea na hivyo kuleta tafsiri mbaya ya chombo hiki na kuathiri mwenendo mzima wa shughuli za Bunge.
Kutokana na maelezo hayo pamoja na masharti ya Kanuni ya 5(1) ya Kanuni za Kudumu za Bunge naagiza kuwa, Wabunge wote wanao jisajili na kasha kutoka ukumbini kwa kususia kushiriki mijadala ya Bunge hawastahili kulipwa posho kwa siku zote ambazo wamekuwa wakijisajili, kuingi au kumbini na kasha kutoka ukumbini.
Huu ndio Mwongozo wangu.
Umetolewa leo 8 Juni, 2016.
Dkt. Tulia Ackson (Mb)
NAIBU SPIKA
Share:

Hon. Saumu Heri Sakala

Hon. Saumu Heri Sakala
Member of Parliment (MP)

Video

Recent Posts