.

..

.

..

.

..

.

..

.

..

Wednesday, August 17, 2016

IJUE SABABU YA MBUNGE WA JIMBO LA TANGA MUSSA MBAROK KUKAMATWA NA POLISI

Share:

IJUE SABABU YA MBUNGE WA JIMBO LA TANGA MUSSA MBAROK KUKAMATWA NA POLISI

Share:

Friday, August 12, 2016

MBUNGE SAUMU SAKALA AMEANZA KUFUATILIA CHANGAMOTO ZA WANANCHI WA DALUNI -TANGA FRESH




 
Mbunge SAUMU SAKALA amenza kufuatilia changamoto alilzokutana nazo katika ziara yake wilayani mkinga katika Kata ya Daluni.
Leo mbunge Sakala amekwenda katika kiwanda cha maziwa cha Tanga Fresh kufuatilia suala la kupelekwa kwa mtungi wa maziwa kero ambayo imekua ikiwalazimu wakazi wa Daluni kupeleka maziwa Maramba mjini.
Akiongea na mkuu wa kitengo cha kusambaza Tenki hizo kwenye vituo ADAM NYEREMBE GAMBA amesema kuwa amefurahishwa na hatua ya mbunge huyo kufuatilia suala hilo lakini kwa sasa Tanga Fresh imekubwa na tatizo la kifedha hivyo kunaugumu wa kutekeleza ombi hilo.
Adam amesema kuweka mtungi ni gharama kubwa sana na pia mitungi hiyo haipatikani hapa nchini, kwani mitungi hiyo inaagizwa kutoka nje ya nchi,hivyo nivigumu kuagiza mtungi mmoja.
Hivyo mkuu huyo wakitengo amewataka wafugaji wa Daluni kupeleka maziwa yao Maramba kama hapo awali walivyo kuwa wakifanya.
Pia kiwanda kipo katika urekebishaji wa mfumo wa maji taka ambao urekebishwaji wake unagharimu pesa nyingi sana ni Zaidi ya milioni 350.
Na wasipo rekebisha mfumo huo kuna hatari ya kiwanda hicjo kufungiwa uzalishaji kwani walishapewa notes na waziri wa mazingira kurekebisha mvumo wao wa maji taka
Pia kutokana upatikanaji wa maziwa mengi katika wakati wa vuli hivyo kiwanda kimepanga kufanya upanuzi wa kiwanda hicho na ujenzi huo utagharimu shilingi bilioni 12,hivyo utaona pesa itakayo tumika ni nyingi.
Hivyo Adam amewataka wakazi wa Kata ya Daluni kuwa wavumilivu katika kipindi hiki ambacho kiwanda cha Tanga fresh kipo katika hali mbaya ya kifedha na pindi mambo yakiwa mazuri watapa Mtungu huo wa Maziwa.

Share:

MBUNGE SAUMU SAKALA AENDELEA NA ZIARA KATA YA DALUNI NA MARAMBA WILYANI MKINGA


Msingi wa ujenzi wa Zahanati ya Kata ya Daluni uliogharimu shilingi Milioni 8 ambao kwa sasa umekwama zaidi ya miaka miwili

Siku ya pili ya ziara ya Mbunge Saumu Sakala katika wilaya mkinga ndani ya kata ya Daluni na Kata ya Maramba ambapo lengo ni kusikliza changamoto mbalimbali zinazo wakumba wananchi wa Wilaya ya Mkinga.
Akianzia katika kata ya Daluni wakazi wa kata hiyo walifurahishwa na ziara ya Mbunge hiyo lakini hawakuacha kumpa changamoto zinazowakabili katika kata yao.
Ambapo changamoto ya Zahanati ndio ilikuwa kubwa ambayo inawafanya wakazi wa kata hiyo kutembea hadi maramba mjini ilikupata huduma hiyo.
Ambapo katika changamoto hiyo Mbunge alitakakujua mwenyekiti amelifuatiliaje suala hilo,hivyo mwenyekiti alitoa tarifa ya kukwama kwa zahanati hiyo.
Mwenyekiti wa kitongoji kata ya Daluni alisema kuwa zahanati hiyo ilipangwa kujengwa lakini mpaka sasa ujenzi huo umeishia kwenye hatua ya msingi na kwa sasa ni miaka miwili imepita kila wakilifuatila suala hilo majibu hakuna.
Pia mwenyekiti huyo alimuambie mbunge kuwa ujenzi huo mpaka sasa umetumia shilingi milioni 8 suala ambalo pia linawaacha wananchi mdomo wazi.
Hatahivyo Mbunge alimtaka mwenyekiti kuatilia tena suala hilo kwani haiwezekani kiasi kikubwa cha pesa kimetumika na zahanati ipo katika hatua ya msingi.
Vilevile katika hatua nyingine wananchi hao wamelalamikia suala la kuto patikana na huduma ya kupatikana kwa vyeti vya kuzaliwa kwa watoto na kusema kuwa wanalazimika kutembea hadi mkinga mjini.
Hivyo walimtaka Mbunge kuwaombea huduma hiyo kusogozewa karibu kwani usumbufu wanaokutana nao ni mkubwa ili kuweza kupata huduma hiyo.
Na kwa upande wake Mbunge Saumu Sakala amewaahidi wakazi wa kata ya Daluni kuwa ataongea na RITA ili kuweza kuwasogezea huduma hiyo karibu wakazi wa daluni hata kwa mwezi mara ,moja ilikuweza kuwaondolea wakazi hao usumbufu huo.
Pia changamoto ya kukosekana kwa Tenki ya kuhifadhiwa maziwa hatua inayosababisha wafugaji wa kata ya Daluni kutembea hadi maramba kupeleka maziwa yao.
Hivyo walimtaka Mbunge awafuatilie suala la hilo katika uongozi wa Tanga Fresh ili waweze kupata Tenki hiyo.
Halikadhalika katika kata ya Maramba vitu vilivyo jitokeza ni kuuzwa kwa mbao ambazo zilikatwa kwa lengo la kutengenezwa kwa mdawati ya shule ya Maramba.
Na changamoto inayo wakwamisha ni kukosa fedha ya nauli ambayo itawafikisha hadi kwa mkurugenzi na mkuu wa wilaya ilikulifuatilia suala la kuuzwa kwa mbao hizo.
Hivyo Mbunge aliwawezesha Fedha ya nauli nakuwaambia kwa kilahatua watakayo fika wamjulishe na pia mbunge amewaahidikuwapa ushirikiano juu ya kutatua suala hilo.
Ziara ya Mbunge Saumu Sakala iliishia katika kata ya Maramba na kata ya Daluni ambapo ameahidi kuyafuatilia yale yote ambao wamempa kwa lengo ya kuyatatua,

Share:

YALIO JIRI ZIARA YA MBUNGE SAUMU SAKALA KATA ZA SIGAYA,BOMA,MKINGA MJINI, NA KATA YA KWALE WILAYANI MKINGA




 
Mbunge Saumu Sakala akikagua Jengo la Shule iliyo Jengwa kupitia nguvu za wananchi katika kata ya Sigaya Wilayani Mkinga





Mbunge Saumu Sakala amendelea na ziara ya kata kwa kata wilaya kwa wilaya katikawilaya ya mkinga kata ya sigaya.
Katika ziara hiyo aliongozana na wenyeviti na diwani wa viti maalum kujua changamoto zinazo wakabili wanakijiji wa kata ya sigaya iliyoko wilaya ya mkinga.
Mbunge amejionea changamoto ya wahamiaji haramu kutoka kenya  inayo wakabili wakazi wa kata hiyo,ambapo wahamiaji hao wamekua wakiharibu mazingira kwa kukata miti na kwenda kuuza kenya.
Wananchi hao pia wamelalamikia suala la wizi wa mifugo unao fanywa na wahamiaji hao huku wakisema wahamiaji ni kutoka kabila la waduruma na wakamba ambao baada ya kuiba mifugo huenda kuuza kenya.
Kunyang’anywa kwa vitambulisho vya ukazi kwa baadhi ya raia ambao ni WATANZANIA huku mamlaka husika wilayani mkinga ikidai ni wahamiaji kutoka kenya.
Pia wananchi wa kata ya sigaya wamelalamikia changamoto ya  kutokamilika kwa shule ya msingi iloiyojengwa kupitia nguvu za wananchi,vyoo pamoja na kutokamilika kwa nyumba za wauguzi katika kata hiyo .
Suala ambalo Mbunge Saumu Sakala amehuzunika sana  hatua ya shule iliyojengwa kupitia nguvu za wananchi na serikali kushindwa kuwasidia wananchi hao kukamilisha shule hiyo.
Lakini kufuatia changamoto hizo Mh Mbunge Saumu Sakala ameahidi kufuatilia matatizo hayo na kuwaambia wana kata ya sigaya kuwa atakutana na Waziri wa mambo ya ndani juu ya kupambana na suala la wahamiaji haramu kutoka kenya.
Pia mbunge saumu sakala aliendelea na ziara yake katika kata tatu ambazi ni kata ya Boma Ndani ,Mkinga Mjini,na kumalizia katika kata ya kwale ambapo alikutana na chamgamotom nyingi ambazo kwanamna moja ama nyingine zinarudisha maendeleo ya wilayaya mkinga.
Miongoni mwa changamoto hizo ni ubovu wa barabara katika kata ya Boma Ndani ambayo kwa wakati wa mvua watoto wa shule huwawanashindwa kwenda shule.
Suala la ambalo Diwani wa Kata hiyo Nasir Salim Saum amesema yuko katika hatua mwisho ya ufuatiliaji kwani mara nyingi amekua akiipigia kelele lakini changamoto ni ilikua pesa hakuna hivyo ameahidiwa na halmashauri kuwa wataifanyia marekebisho barabara hiyo.
Hatahivyo kwa upande wa Mbunge Saumu Sakala amewaambia wananchi katika kata hiyo wawe kitu kimoja katika kuijenga kata yao na pele wanaona ugumu wasiache kumshirikisha kwani nyeye yupo kwaajili ya kuwatumukia wao.
Share:

Thursday, August 11, 2016

NORA PENDAELI AKIELEZEA JUU YA SHIRIKA LA IRI Katika kikao cha wanawake ...

Share:

KWAKAULI MOJA TUSEME NDOA ZA UTOTONI BASI



Shirika lisilo la kiserikali la International Republican Institute (IRI) likishirikiana na Mbunge wa vitimaalum Pangani Mh saumu sakala leo wamefanya kikao na wakinamama wilayani pangani na lengo likiwa ni kuangalia usalama wa mtoto wa kike kwa ujumla.

Akiongea katika kiao hicho Mbunge Saumu Sakala amesema kuwa wameamu kukaa na kinamama wilaya ya pangani kutoka na hali ya ukatili wanao fanyiwa  watoto wakike katika jamii,ikiwemo ndoa za utotoni sambamba na mimba za utotoni.
Kikao hicho pia kimehusisha kuiangalia sharia ya ndoa ambayo kwa kipindi chote ilikua ikimbana mtoto wakike ,ambayo sharia hiyo ilikua inaruhusu mtoto wa kike kuolewa kuanzia miaka 15.
Mh sakala ameongezea kuwa sharia hiyo ndio chanzo cha mimba za utotoni ambayo madhra yake ni mwakubwa kwanza kwa mtoto wa kike na pili kwa mtoto anaye mzaa,hivyo aliwataka wanawake kujadili kwa ilikupata njia thabiti  ya kumlinda mtoto wa kike kwa maendeo ya Taifa.
Pia Muweezeshaji kutoka shirika la IRI NORA PENDAELI aliwakaribisha wakinamama wa pangani kutoa mchango wao kuhakikisha wazazi wanamlinda mtoto wa kike na kutokomeza janga la ndoa za katika umri mdogo.
Akichangia katika kikao hicho CHAUSIKU JUMA alisema ili kumlinda mtoto wakike ni lazima kinamama kuwa kitu kimoja na kuona kuwa mtoto wa mwenzako ni kama mtoto wako kwakufnya hivyo kutamfanya mtoto wa kike kuwa salama.
Kwani maswahibu mengi yanayompata mtoto wa kike katika jamii ni kwakua wazazi hawana umoja kila mzazi siku hizi humuangalia mtoto wake, hivyo kuwapa mwanya wanaume kuwarubuni na kuwasababishia mimba watoto wakike.
CHAUSIKU ameongezea kuwa katika suala la ndoa za utotoni zinaathari kubwa kwa watoto wakike kwani mtoto wa kike mwili wake unakua hauja komaa kwahiyo madhara anaweza kuyapata katika kujifungua,hivyo sio vizuri kwa kinamama kuwaoza watoto wakike katikaumri mdogo.
Hata hivyo mchangiaji wa pili AISHA MSOFE amesema kuwa licha ya madhara ya ndoa za utotoni kuwa na athari kwa mtoto wakike lakini pia athari inakuja katika familia kwani familia inabeba mzigo mkubwa baada ya mtoto wa kike kuachika katika ndoa.
Pia alisisitiza kuwa shariaya ndoa  inayotakiwa kufanyiwa marekebisho ifike hatua serikali iitekeleze matakwa ya sharia mpya itakayo pita kwa vitendo  kwani mara nyingi imekua ikiishia kwenye vitabu tu na kwaupande wa utekelezaji unakua mdogo.
ZAINABU YASINI mchangiaji katika kikao hicho amesema kuwa katika eneo la pangani matukio mengi ya yanayo wakumba wanawake yanashindwa kuchukuliwa hatua kutokana  na sababu ya kuweka udugu mbele.
Hivyo utakuta mtoto wa kike kapatiwa mimba na mtoto wakiume lakini mamamzazi wa wa mtoto wakike anashindwa kulipeleka suala mahakamani kisa alie sababisha ujauzito ni mtoto wa jirani.
Hata hivyo suala la elimu pia limeongele ambapo mchangiaji SOFIA MZINGA amesema kuwa kufanyike kwa warsha na semina mara kwa mara kwa ajili ya kuwahamasisha wazazi juu ya kuwalinda watoto wa kike ,kwakufanya hivyo itasaidia kupunguza matukio ya mimba za utotoni.
Na katika kuchingia suala la mimba za utotoni Mh SAUMU SAKALA amesema wazazi wananafasi kubwa ya kuzuzi tatizo hilo kwani wanakaa sana na watoto hivyo wakiongea nao vizuri na kuwaeleza madhara ya mimba katika umri mdogo watoto hawatashawishika.
Pia Mh SAUMU SAKALA ameahidi kuyapeleka katika bunge la Jamuhuri ya Muungano Wa Tanzania yale yote kinamama waliyo yaomba kwa niaba ya kumlinda mtoto wakike kwa manufaa ya Taifa.
Hata hivyo kikao hicho kimeadhimia kuanzisha jukwaa la kinamama kwa ajili ya kujadili mipango mbalimbali lengo likiwa ni kuhakikisha mtoto wa kike anapiga hatua mbele kwakupinga ndoa katika umri mdogo samaba na matumizi ya dawa za kulevya.
Share:

Hon. Saumu Heri Sakala

Hon. Saumu Heri Sakala
Member of Parliment (MP)

Video

Recent Posts