Shirika
lisilo la kiserikali la International Republican Institute (IRI) likishirikiana
na Mbunge wa vitimaalum Pangani Mh saumu sakala leo wamefanya kikao na
wakinamama wilayani pangani na lengo likiwa ni kuangalia usalama wa mtoto wa
kike kwa ujumla.

Kikao
hicho pia kimehusisha kuiangalia sharia ya ndoa ambayo kwa kipindi chote ilikua
ikimbana mtoto wakike ,ambayo sharia hiyo ilikua inaruhusu mtoto wa kike
kuolewa kuanzia miaka 15.
Mh
sakala ameongezea kuwa sharia hiyo ndio chanzo cha mimba za utotoni ambayo
madhra yake ni mwakubwa kwanza kwa mtoto wa kike na pili kwa mtoto anaye
mzaa,hivyo aliwataka wanawake kujadili kwa ilikupata njia thabiti ya kumlinda mtoto wa kike kwa maendeo ya
Taifa.
Pia
Muweezeshaji kutoka shirika la IRI
NORA PENDAELI aliwakaribisha wakinamama wa pangani kutoa mchango wao
kuhakikisha wazazi wanamlinda mtoto wa kike na kutokomeza janga la ndoa za
katika umri mdogo.
Akichangia
katika kikao hicho CHAUSIKU JUMA alisema ili kumlinda mtoto wakike ni lazima
kinamama kuwa kitu kimoja na kuona kuwa mtoto wa mwenzako ni kama mtoto wako
kwakufnya hivyo kutamfanya mtoto wa kike kuwa salama.
Kwani
maswahibu mengi yanayompata mtoto wa kike katika jamii ni kwakua wazazi hawana
umoja kila mzazi siku hizi humuangalia mtoto wake, hivyo kuwapa mwanya wanaume
kuwarubuni na kuwasababishia mimba watoto wakike.
CHAUSIKU
ameongezea kuwa katika suala la ndoa za utotoni zinaathari kubwa kwa watoto
wakike kwani mtoto wa kike mwili wake unakua hauja komaa kwahiyo madhara
anaweza kuyapata katika kujifungua,hivyo sio vizuri kwa kinamama kuwaoza watoto
wakike katikaumri mdogo.
Hata
hivyo mchangiaji wa pili AISHA MSOFE amesema kuwa licha ya madhara ya ndoa za
utotoni kuwa na athari kwa mtoto wakike lakini pia athari inakuja katika
familia kwani familia inabeba mzigo mkubwa baada ya mtoto wa kike kuachika
katika ndoa.
Pia
alisisitiza kuwa shariaya ndoa inayotakiwa kufanyiwa marekebisho ifike hatua
serikali iitekeleze matakwa ya sharia mpya itakayo pita kwa vitendo kwani mara nyingi imekua ikiishia kwenye
vitabu tu na kwaupande wa utekelezaji unakua mdogo.

Hivyo
utakuta mtoto wa kike kapatiwa mimba na mtoto wakiume lakini mamamzazi wa wa
mtoto wakike anashindwa kulipeleka suala mahakamani kisa alie sababisha
ujauzito ni mtoto wa jirani.
Hata
hivyo suala la elimu pia limeongele ambapo mchangiaji SOFIA MZINGA amesema kuwa
kufanyike kwa warsha na semina mara kwa mara kwa ajili ya kuwahamasisha wazazi
juu ya kuwalinda watoto wa kike ,kwakufanya hivyo itasaidia kupunguza matukio
ya mimba za utotoni.
Na
katika kuchingia suala la mimba za utotoni Mh SAUMU SAKALA amesema wazazi wananafasi
kubwa ya kuzuzi tatizo hilo kwani wanakaa sana na watoto hivyo wakiongea nao
vizuri na kuwaeleza madhara ya mimba katika umri mdogo watoto hawatashawishika.
Pia
Mh SAUMU SAKALA ameahidi kuyapeleka katika bunge la Jamuhuri ya Muungano Wa
Tanzania yale yote kinamama waliyo yaomba kwa niaba ya kumlinda mtoto wakike
kwa manufaa ya Taifa.
Hata
hivyo kikao hicho kimeadhimia kuanzisha jukwaa la kinamama kwa ajili ya
kujadili mipango mbalimbali lengo likiwa ni kuhakikisha mtoto wa kike anapiga
hatua mbele kwakupinga ndoa katika umri mdogo samaba na matumizi ya dawa za
kulevya.